……………………………..
WAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Benard Membe anatarajia kuwa mgeni rasmi kwenye Tamasha la Qaswida lililoandaliwa na Ulamaa Promotions Centre litakalofanyika Mei 24 kwenye viwanja vya sekondari ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi ya tamasha hilo, ustadh Jumanne Ligopora
Ligopora alisema wamejipanga katika tamasha hilo kushirikisha madrasa zaidi ya 50 za jijini Dar es Salaam na baadhi ya mikoa.
Aidha Ligopora alisema hivi sasa wako kwenye mchakato wa kusambaza mialiko kwa madrasa za Dar es Salaama na mikoani.
“Tunatarajia maelfu ya Waislamu kumiminika kwa wingi katika viwanja vya Benjamin Mkapa kwa lengo la kupata ladha mbalimbali za Qaswida,” alisema Ligopora,” alisema Ligopora.
Mwenyekiti huyo wa Kamati ya maandalizi, alisema wameshapeleka taarifa kwa madrasa mbalimbali za jijini Dar es Salaam na nyingine zilizoko mikoa jirani.