$ 0 0 Meneja Uragibishi na Mawasiliano wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo, WAMA, Ndugu Philomena Marijani (aliyesimama)akitoa maelezo mafupi kuhusu semina ya siku 5 kwa wanafunzi wa Shule za Sekondari katika Wilaya ya Temeke itayozungumzia uzuiaji wa mimba za utotoni kwa wanafunzi wa wilaya hiyo. Semina hiyo inafanyika katika Shule ya Sekondari Kibasila kuanzia tarehe 13 hadi 17.4.2015.(PICHA NA JOHN LUKUWI). Baadhi ya wanafunzi na walimu kutoka Shule 11 za Sekondari katika Wilaya ya Temeke wakisikiliza hotuba ya mgeni rasmi, Afisa Elimu-Sekondari wa Wilaya ya Temeke Ndugu Donald Chavila (hayuko pichani) wakati alipokuwa akifungua rasmi semina ya siku tano inayozungumzia uzuiaji wa mimba za utotoni kwa wanafunzi wa Wilaya hiyo tarehe 13.4.2015 kwenye ukumbi wa sherehe wa Kibasila Sekondari.Afisa Elimu-Sekondari wa Wilaya ya Temeke Bwana Donald Chavila akifungua rasmi semina ya siku 5 ya kuzuia mimba za utotoni kwa wanafunzi wa Shule za Sekondari katika Wilaya ya Temeke. Semina hiyo inaendeshwa na Taasisi ya WAMA, ikishirikiana na Shirika la Engender Health la Marekani na kufadhiliwa na Shirika la Misaada la Serikali ya Marekani,USAID.Baadhi ya wanafunzi na walimu wa Shule za Sekondari kutoka Wilaya ya Temeke wakifuatilia kwa makini hotuba ya Mgeni rasmi, Afisa Elimu-Sekondari wa Wilaya ya Temeke Ndugu Donald Chavila wakati akifungua semina hiyo inayofanyika Kibasila Sekondari. Baadhi ya wanafunzi kutoka Shule za Sekondari katika Wilaya ya Temeke wakisikiliza kwa maini baadhi ya mada zilizokuwa zikitolewa wakata wa semina ya kuzuia mimba za utotoni kwa wanafunzi wa Sekondari katika wilaya hiyo. Semina hiyo ya siku 5 inafanyika Kibasila Sekondari na ilifunguliwa rasmi tarehe 13.4.2015.Washiriki wa semina wakiwa wamegawanyika katika vikundi mbalimbali ili kujadili mojawapo ya mada iliyokuwa imetolewa na baadaye kila kundi kuwasilisha kwenye semina hiyo.Washiriki wa semina wakiwa wamegawanyika katika vikundi mbalimbali ili kujadili mojawapo ya mada iliyokuwa imetolewa na baadaye kila kundi kuwasilisha kwenye semina hiyo.Mwanafunzi mshiriki wa semina ya kuzuia mimba za utotoni kwa wanafunzi wa shule za sekondari katika Wilaya ya Temeke akiwasilisha majibu ya majadiliano ya kikundi chao katika siku ya kwanza ya semina hiyo.