Baadhi ya mashamba ya migomba yaliyofyekwa na kijiji kwa madai kuwa shamba hilo lipo ndani ya eneo la kijiji,
Baadhi ya wahanga waliovunjiwa nyumba zao wakiwa katika mabaki ya nyumba hizo ,katika kijiji cha Sakila wilayani Arumeru.
FAMILIA saba zenye watu zaidi ya 30 katika kijiji cha Sakila,wilayani Arumeru mkoani hapa,hazina mahala pa kuishi kutokana na nyumba zao kubomolewa na mwenyekiti wa kijiji hicho kwa madai kuwa zilijengwa bila kufuata utaratibu.
Aidha familia hizo wakiwemo watoto wadogo zimelazimika kulala kwenye mabaki ya nyumba hizo licha ya baridi kalli na mvua zinazonyesha wilayani humo baada ya kukosa mahala pa kujikimu.
Akizungumzia kadhia hiyo mmoja wa wahanga hao,Samson Joseph Nasary(70) alisikitishwa na hatua ya mwenyekiti wao Richard Mbise akiwa na kundi la watu zaidi ya 20 kuvamia makazi yao na kubomoa nyumba zao huku wakimwaga akiba kidogo ya chakula walichokuwa nacho .
Alisema tukio hilo limetokea April 2 mwaka huu ambapo askari wa kampuni ya ulinzi ya Kifaru ndio walikuwa wakitekeleza zoezi hilo wakiongozwa na uongozi wa kijiji hicho.
‘’Eneo hilo ni mali ya baba yetu mzee Joseph Mareu Nasary aliyeishi hapa tangu mwaka 1948 na baada ya kufariki alituachia urithi tukiwa tunaishi hapa,wakati kijiji kinaanza mwaka 1976 /77 sisi tayari tunaishi hapa sasa tunasikitika sana leo hii kuvamiwa na kuvunjiwa nyumba zetu wakisema eti tumevamia’’alisema
Naye mkazi mwingine Peter Mafie alilalamikia hatua ya mwenyekiti huyo kuamuru kufyekwa kwa migomba yake na mazao aliyootesha kwenye shamba lake bila kushirikishwa .
Alieleza kuwa kabla ya kumchagua mwenyekiti wao,aliwahidi kuwa angewasaidia kutatua mgogoro huo bila kuondolewa kwenye makazi yao,suala ambalo lilichangia wao kumchagua kwa kishindo.
Hata hivyo wameshangaa baada ya kumchangua amewageuka na kubomoa nyumba zao.
Wengine waliobomolewa nyumba zao ni,Lightnes Charles ambaye ni mjane,David Israel,Lucas Akyo ,Visenti Mathias ,Joshua Shayo,Deatres Sakwera na Selian Juma wote wakazi wa kijiji hicho.
Aidha wameitaka serikali akiwemo mbunge wao Joshua Nasary kuwasaidia wapate haki yao ya kurejeshewa makazi hayo kwani kwa sasa wanaishi kwa kubangaiza na kulala mahala pasipo stahili.
Kwa upande wa mwenye kiti,Richard Mbise alikiri kubomoa nyumba za wakazi hao akisisitiza kuwa alikuwa akitekeleza amri ya mahakama ya ardhi ya wilaya iliyotoa ushindi kwa kwa uongozi wa kijiji.
Hata hivyo alisisitiza kuwa wananchi hao walivamia eneo hilo lililotengwa kwa ajili ya huduma mbalimbali za kijiji ikiwemo ujenzi wa zahanati na shule na kuanzisha makazi.
Aliongeza kuwa uongozi wa kijiji ulijaribu mara kadhaa kuwaondoa katika eneo hilo lakini walikuwa wakaidi hadi suala hilo walipoamua kulifikisha mahakamani.
habari na libeneke la kaskazini blog
Baadhi ya mashamba ya migomba yaliyofyekwa na kijiji kwa madai kuwa shamba hilo lipo ndani ya eneo la kijiji,
Baadhi ya wahanga waliovunjiwa nyumba zao wakiwa katika mabaki ya nyumba hizo ,katika kijiji cha Sakila wilayani Arumeru.
FAMILIA saba zenye watu zaidi ya 30 katika kijiji cha Sakila,wilayani Arumeru mkoani hapa,hazina mahala pa kuishi kutokana na nyumba zao kubomolewa na mwenyekiti wa kijiji hicho kwa madai kuwa zilijengwa bila kufuata utaratibu.
Aidha familia hizo wakiwemo watoto wadogo zimelazimika kulala kwenye mabaki ya nyumba hizo licha ya baridi kalli na mvua zinazonyesha wilayani humo baada ya kukosa mahala pa kujikimu.
Akizungumzia kadhia hiyo mmoja wa wahanga hao,Samson Joseph Nasary(70) alisikitishwa na hatua ya mwenyekiti wao Richard Mbise akiwa na kundi la watu zaidi ya 20 kuvamia makazi yao na kubomoa nyumba zao huku wakimwaga akiba kidogo ya chakula walichokuwa nacho .
Alisema tukio hilo limetokea April 2 mwaka huu ambapo askari wa kampuni ya ulinzi ya Kifaru ndio walikuwa wakitekeleza zoezi hilo wakiongozwa na uongozi wa kijiji hicho.
‘’Eneo hilo ni mali ya baba yetu mzee Joseph Mareu Nasary aliyeishi hapa tangu mwaka 1948 na baada ya kufariki alituachia urithi tukiwa tunaishi hapa,wakati kijiji kinaanza mwaka 1976 /77 sisi tayari tunaishi hapa sasa tunasikitika sana leo hii kuvamiwa na kuvunjiwa nyumba zetu wakisema eti tumevamia’’alisema
Naye mkazi mwingine Peter Mafie alilalamikia hatua ya mwenyekiti huyo kuamuru kufyekwa kwa migomba yake na mazao aliyootesha kwenye shamba lake bila kushirikishwa .
Alieleza kuwa kabla ya kumchagua mwenyekiti wao,aliwahidi kuwa angewasaidia kutatua mgogoro huo bila kuondolewa kwenye makazi yao,suala ambalo lilichangia wao kumchagua kwa kishindo.
Hata hivyo wameshangaa baada ya kumchangua amewageuka na kubomoa nyumba zao.
Wengine waliobomolewa nyumba zao ni,Lightnes Charles ambaye ni mjane,David Israel,Lucas Akyo ,Visenti Mathias ,Joshua Shayo,Deatres Sakwera na Selian Juma wote wakazi wa kijiji hicho.
Aidha wameitaka serikali akiwemo mbunge wao Joshua Nasary kuwasaidia wapate haki yao ya kurejeshewa makazi hayo kwani kwa sasa wanaishi kwa kubangaiza na kulala mahala pasipo stahili.
Kwa upande wa mwenye kiti,Richard Mbise alikiri kubomoa nyumba za wakazi hao akisisitiza kuwa alikuwa akitekeleza amri ya mahakama ya ardhi ya wilaya iliyotoa ushindi kwa kwa uongozi wa kijiji.
Hata hivyo alisisitiza kuwa wananchi hao walivamia eneo hilo lililotengwa kwa ajili ya huduma mbalimbali za kijiji ikiwemo ujenzi wa zahanati na shule na kuanzisha makazi.
Aliongeza kuwa uongozi wa kijiji ulijaribu mara kadhaa kuwaondoa katika eneo hilo lakini walikuwa wakaidi hadi suala hilo walipoamua kulifikisha mahakamani.
habari na libeneke la kaskazini blog