Banda la Jeshi la Magereza lililopo katika Viwanja vya Maonesho ya Biashara ya Kimataifa, Jijini Dar es Salaam. Jeshi la Magereza linashiriki katika Maonesho ya 38 ya Biashara Mwaka 2014 ambapo Wananchi wanakaribishwa kuja kutembelea Banda la Jeshi la Magereza ili waweze kupata bidhaa mbalimbali za Samani za ndani zenye ubora wa hali ya juu pamoja na bidhaa nyinginezo za ngozi zinazozalishwa na Jeshi la Magereza.Sofa seti iliyotengenezwa kwa Ustadi mkubwa na Mafundi Stadi wa Jeshi la Magereza kama inavyoonekana katika picha. Sofa hiyo imetengenezwa kwa kutumia Mbao aina ya Mkongo ambao ni imara na hudumu kwa muda mrefu zaidi.