Mchezaji wa zamani wa klabu ya Barcelona Patrick Kluivert akiwaongoza wachezaji wenzake akiwepo Simao Sabrosa muda mfupi mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA)
Wachezaji wa Barcelona wakielkea upande wa watu mashuhuri katika uwanja wa ndege wa Kiamtaifa wa Kilimanjaro (KIA)
Mchezaji Luis Garcia(kulia) akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro .kushoto ni mratibu wa safari ya wachezaji wa zamani wa klabu ya Barcelona Royco Garcia.
Wachezaji wa zamamni wa klabu ya Barcelona wakijadiliana jambo katika uwanja wa ndege wa Kilimanjaro muda mfupi mara baada ya kuwasili na ndege ya shirika la ndege la KLM.
Simao Sabrosa mchezaji wa zamani wa klabu ya Barceona akiwa katika eneo la mapumziko katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro.
Mchezaji Patrick Kluivert akizingumza kwa simu muda mfupi mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro KIA jana usiku .
Meneja maendeleo wa KiboPalace Hotel ,Charity Githinji akiteta jambo na wachezaji wa zamani wa klabu ya Barcelona walioanza kuwasili nchini kwa ajili ya mchezo wa kirafiki dhidi ya wachezaji wa zamani wa Tanzania.