Quantcast
Channel: ARAWAY MEDIA TANZANIA
Viewing all articles
Browse latest Browse all 6856

CHIKAWE ACHUKUA FOMU YA KUOMBA KUTEULIWA KUGOMBEA URAIS 2015

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Mathias Chikawe (katikati) akionyesha kabrasha lenye fomu ya kuomba kuteuliwa kugombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM). Kushoto ni Katibu wa Halmashauri Kuu Taifa (Nec) ya CCM wa Idara ya Oganizesheni, Dk. Mohamed Seif Khatibu. Kulia ni mkewe Waziri Chikawe, Profesa Amandina Lihamba. Tukio hilo la uchukuaji wa fomu lilifanya katika Ofisi za Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma jana.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Mathias Chikawe akiwaonyesha wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na waandishi wa habari (hawapo pichani) kabrasha lenye fomu ya kuomba kuteuliwa kugombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CCM kabla ya kuanza kuzungumza na kujibu maswali mbalimbali ya waandishi wa habari. Kulia ni mkewe Waziri Chikawe, Profesa Amandina Lihamba. Tukio hilo la uchukuaji wa fomu lilifanya katika Ofisi za Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma jana.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Mathias Chikawe akizungumza na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) pamoja na waandishi wa habari mara baada ya kuchukua fomu ya kuomba kuteuliwa kugombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CCM, Waziri Chikawe ambaye alijibu maswali ya waandishi wa habari kiufasaha huku akishangiliwa na wanachama hao, alisema yeye ni kiongozi mwenye uzoefu mkubwa na pia akiteuliwa na chama chake kugombea nafasi hiyo ataendeleza mapambana zaidi dhidi ya maadui watatu ambao ni ujinga, maradhi na umaskini pamoja na adui mwingine rushwa ambaye ni adui wa maendeleo. Kulia ni mkewe, Profesa Amandina Lihamba.(Muro)

Viewing all articles
Browse latest Browse all 6856

Trending Articles